Friday, August 1, 2014

Dk Kamani amwaga misaada jimbo la Busega






Dk Kamani amwaga misaada jimbo la Busega

Na Antony Sollo Busega.

Julai 24.2014

Mbunge wa jimbo la Busega ambaye  pia ni WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Dk Titus Kamani amemwaga mamilioni katika Jimbo la Busega Mkoani Simiyu ikiwa niutekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi pamoja na ahadi alizotoa wakati wa kuomba ridhaa kwa wananchi katika Uchaguzi Mkuu wa 2010.

Dk Kamani amezindua miradi mbalimbali jimboni humo ambapo kati ya miradi hiyo ni mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa halmashauri ya wailaya ya Busega utakaogharimu shilingi milioni 500,000,000.

Akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kata ya Mwamanyili Nassa jineri Dk Kamani aliwashukuru wananchi nkwa kumchagua kuwa Mbunge wa Jimbo la Busega.

“Ndugu zangu naomba kuwapongeza kwa mambo matatu,nawapongezeni sana kwa kunichagua kuwa Mbunge wenu,pili kwa kujitokeza kwa wingi katika ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi pamoja na ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Jakaya Kikwete kwa ajili ya uzinduzi wa Mkoa wetu mpya wa Simiyu”.

Kuhusu Makao Makuu ya Wilaya Dk Kamani alisema kuwa namshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa kuichagua Wilaya ya Busega kuwa Makao Makuu ya Wilaya ambapo Kata ya Mwamanyili lakini pia kwa uamzi wake wa kumalizia ziara yake Katika Wilaya ya Busega ambapo ziara hiyo imezaa matunda mengi kwa kuelekeza miradi mbalimbali inayoendelea hadi sasa.

Nawapongeza pia kwa kuwa tayari kutoa maeneo kwa ujenzi wa nyumba za watumishi wa halmashauri lakini pia mtafanya biashara kwa kuwa Makao makuu yako katika maeneo yenu,hongereni sana.

Kuhusu elimu Dk Kamani alisema kuwa,tangu aingie madarakani amesimamia ujenzi wa Sekondari tatu ambapo amezitaja shule hizo kuwa ni Mwasamba,Mwamagigisi na Kijirimi.

Dk Kamani ameahidi kupeleka umeme wa jua katika ya Msingi Kishamapanda,na pia aliwapongeza wananchi wa Nyang’hanga kwa uamzi wao wa kujitolea kujenga shule na kuahidi kuchangia shilingi 500,000 kwa ajili ya ujenzi wa choo na mabati 100.

Mwisho



Dk Kamani akizungumza na wazee wa Kijiji cha Yitwimila muda mfupi baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Ofisi ya Kijiji hicho

Dk Kamani akikagua jengo la Ofisi ya Kijiji cha Yitwimila lililojengwa na wananchi

Dk Titus Kamani alipowasili kukagua mradi wa umeme  huko Nyangili julai 25 2014

Dk Kamani akiwa na mjumbe wa Mkutano wa Mkoa simiyu kabla ya kuhutubia mkutano wa wananchi

Dk Titus Kamani akipata taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa kijiji kabla ya kufungua mradi wa maji 

Dk Titus Kamani akifurahia jambo baada ya kusikiliza kikundi cha ngoma wakati wa zira yake katika kata ya Nyangili Busega.
Dk Kamani akiangalia vifaa vinavyotumika kufunga umeme katika mradi wa REA unaotekelezwa jimboni Busega.

Dk Kamani akimsikiliza Katibu wa CCM Wilaya ya Busega baada ya kukagua mradi wa umeme vijijini REA jimboni Busega Picha na Antony Sollo Tanzania Daima

Dr Kamani  akiwa na viongozi mbalimbali katika jimbo la Busega akiwa na ziara ya kukagua nmiradi mbalimbali jimboni humo julai 24 2014. Picha zote na Antony Sollo wa Tanzania Daima.

0 comments:

Post a Comment