Thursday, June 26, 2014

Boda boda Usagara hawana Leseni

Boda boda Usagara hawana Leseni

Na Antony Sollo Mwanza.
26june 2014

WAENDESHA Pikipiki wengi Usagara hawana leseni imefahamika,akizungumza na waendesha bodaboda katika Mtaa wa Usagara eneo la Mizani Afisa wa Jeshi la Polisi CPL Bakari Mwakipiko alibainisha kuwepo kwa waendesha bodaboda wengi ambao hawana leseni ya udereva na pia wakiwa hawajui sheria za Usalama barabarani.  

Bakari alisema kuwa amesikitishwa na ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani unaofanywa na waendesha pikipiki hao na kusema kuwa hicho ni chanzo kikubwa cha ongezeko la ajali nchini kwa kuwa vijana hao wanaponunua pikipiki hizo tu huingia barabarani na kuanza kuendesha bila kupata mafunzo ya aina yoyote jambo ambalo amekemea vikali.

Bakari amesema kuwa Serikali itawachukulia hatua kali wale watakaoendelea kukaidi maelekezo ikiwemo kupata mafunzo ya uendeshaji wa vyombo hivyo pamoja na leseni  za kuendeshea.
“Nawaonya haya mambo ya uvunjaji wa sheria sasa yamefikia mwisho,tumewaangalia muda mrefu maana mmekuwa mkifanya mambo yenu kama kwamba serikali haipo,sheria inawataka muendeshe vyombo hivi mkiwa mmevaa kofia,lakini pia kubeba abiria kufuatana na maelekezo ya mtengenezaji wa chombo” alisema Bakari.

Serikali imetambua kazi yenu kuwa ni ajira kwa mujibu wa sheria nawashangaa mnapokiuka kanuni na taratibu zilizowekwa mnataka tuwafanye nini?alihoji CPL Bakari.

Nawaomba muunde uongozi ili muweze kutambulika katika eneo lenu kisheria,na muweze kusaidiwa na mifuko yenu mtakayokuwa mnachangishana ili hata kama mmoja wenu atapata matatizo aweze kupata msaada.

Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza limeendelea kutoa elimu kwa waendesha Pikipiki maarufu Bodaboda ili kupunguza ajari za barabarani huku tafiti mbalimbali zikionyesha kuwa chanzo cha ajari nchini ni waendesha pikipiki na waendesha baiskeli.

0 comments:

Post a Comment