Na Antony Sollo Misungwi.
AFISA
Mtendaji wa Kijiji cha Sanjo Charles Bulugu,amemchongea kwa Mkuu wa Wilaya ya
Misungwi Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Eliud Mwaiteleke baada ya kutoa taarifa
za uongo katika mkutano wa Serikali ya Kijiji cha Sanjo uliofanyika August 18 mwaka huu akisema kuwa,Mkurugenzi huyo ameshindwa kufika
kijijini hapo kwa kukosa gari la kumpeleka kusikiliza kero za wananchi hao.
Ilidaiwa
kuwa Mkuu huyo wa Wilaya alitoa agizo hilo kufuatia malalamiko yaliyotolewa na
wananchi wa Kijiji cha Sanjo kuomba Uongozi wa Wilaya ya Misungwi ufike hapo
kwa ajiri ya kusikiliza kero zao.
Akitoa
taarifa hizo Bulugu alisema kuwa Mkurugenzi amekwama kufika katika mkutano huo
kutokana na kukosa usafiri kufuatia gari lake kuwepo katika usimamizi wa
mitihani ya Taifa kwa wanafunzi wa Darasa la Saba.
“Ndugu
zangu wananchi kwa niaba ya Mkurugenzi
napenda kuwaomba radhi kwa kuchelewa kufika hapa mgeni wetu sasa ni saa
tano asubuhi ,ni kwamba mgeni wetu hataweza kufika kutokana na kukosa usafiri
wa kumleta hapa,gari lake liko kwenye shughuli za Mitihani ya Darasa la
saba”alisema Bulugu huku miguno na maswali toka kwa wananchi vikitawala
“Hivi
Mtendaji huoni kuwa huu ni uzembe wa makusudi,magari yote ya Halmashauri hayapo
kweli? hata gari lake liko kwenye mitihani?mbona hawa watu wanataka kuturudisha
tulikotoka? Sasa tunakuagiza Mtendaji ukamwambie Mkuu wa Wilaya kuwa agizo lake
limepuuzwa! kwa nini Mkurugenzi asije hata na Hiece?” alihoji mmoja wa wananchi
waliokuwepo katika mkuitano huo.
Uchunguzi
uliofanywa na MwanaHALISI umebaini kuwa, taarifa hizo hazikuwa za kweli kwani
Mkurugenzi huyo alikuwa safari ya kikazi Mjini Dodoma.
Baada ya
taarifa hiyo wananchi walionyesha kukasirishwa na kitendo hicho na kuahidi
kugomea mikutano ijayo iwapo hawatapata maelezo ya kutosha juu ya tukio hilo.
MwanaHALISI
lilimtafuta Mkurugenzi huyo ili kutolea ufafanuzi wa taarifa iliyotolewa na
Afisa Mtendaji huyo ambapo Mwaiteleke alisema kuwa habari hizo si za kweli
“Mimi kwa
sasa niko Mbeya,nimeshtushwa sana na taarifa hizo mimi nikose usafiri si
ningeenda na pikipiki? Sisi kazi yetu ni moja tu nayo ni kuwatumikia wananchi
na si vinginevyo sijui Mtendaji huyo kapata wapi maelekezo hayo ngoja
nifuatilie”alisema Mwaiteleke.
Wakizungumza
na MwanaHALISI kwa nyakati tofauti wananchi hao walisema kuwa wamekwazwa na
kitendo cha Mkurugenzi kushindwa kufika kijijini jambo walilosema bila
kumung’unya maneno kwamba ni uzembe.
Mwenyekiti
wa Kitongoji cha Nyasubi Meni Lutandula ameliambia MwanaHALISI kuwa kuna udanganyifu mkubwa katika ujenzi wa
tenki la maji katika kijiji cha Sanjo ambapo walibaini matumizi mabaya ya fedha
za wananchi kiasi cha shilingi 20,828,502;60 katika ujenzi wa mradi wa maji.
“Inasikitisha kuna ujenzi wa shule lakini nayo
haijaanza kufanya kazi lakini tayari vyumba vimechakaa na tayari sisi wananchi
tumeshaambiwa kuchangia shilingi 6500 kila familia kwa ajiri ya ukarabati wa
vyumba hivyo”.alisema Lutandula.
Mwenyekiti
wa Kijiji cha Sanjo Bukali John alipotakiwa kutolea ufafanuzi sakata la ujenzi
wa madarasa hayo kujengwa chini ya kiwango alisema kuwa si vizuri kufuatilia
jambo hilo kwa kuwa wananchi tayari wameshakubali kuchangia fedha kwa ajiri ya
kurekebisha vyumba hivyo.
“ Ndugu
mwandishi ni kweli kuna mapungufu yaliyojitokeza katika ujenzi wa vyumba hivyo
lakini nashauri usifuatilie suala hilo maana tayari tumeshafanya vikao na
wananchi na kukubaliana kuchangia fedha kiasi cha shilingi 6500 ili tukarabati
vyumba hivyo” alisema Bukali.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Juma Sweda alisema kuwa hana taarifa
zozote juu ya agizo hilo na kwamba yeye hajawahi kufanya ziara katika kijiji
cha Sanjo
“Mimi
sijawahi kufanya ziara yoyote katika kijiji hicho isipokuwa nilishiriki kikao
cha Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Fela hivyo sijui Afisa Mtendaji huyo alitoa
wapi maelekezo hayo nitafuatilia kujua zaidi juu ya jambo hilo”alisema Sweda.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment