Sunday, August 10, 2014

Chita FC wakilalamikia Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Misungwi

Na Antony  Sollo  Mwanza.
August 08 2014.

Timu  ya  Chitah FC yenye makao yake katika kijiji cha Ng’ombe Kata ya Igokelo,imeulalamikia uongozi  wa chama cha Mpira wa miguu  Wilayani Misungwi MDFA kwa kile ilichodai kufanyiwa  utapeli wakati wa kushiriki ligi daraja la nne iliyomalizika hivi karibuni Wilayani humo.

Akizungumza na Tanzania Daima Mwenyekiti wa Chitah FC Emanuel Saba kalezu alisema,timu hiyo ilionekana kuwa na wachezaji bora,wenye  mvuto na wenye  kujituma katika mchezo  wa mpira wa miguu Wilayani Misungwi.

Emanuel alifafanua kuwa,baada ya timu hiyo kuwa kivutio kwao,Viongozi  wa Wilaya ya Misungwi waliwashawishi wachezaji hao kushiriki ligi hiyo kwa hila ili kuwaingiza katika mzunguko wa ligi daraja la nne ngazi ya Wilaya hiyo huku wakijua fika kwamba timu hiyo haikuwa na leseni ya kushiriki michuano hiyo.

Mwenyekiti huyo aliwataja viongozi waliotumia ujanja ujanja huo kuitapeli timu hiyo kuwa ni Hassan Mwakami Katibu wa  MDFA Wilaya ya Misungwi na Msaidizi wake  Sylivester Nyanda.

Imedaiwa kuwa timu  hiyo ilikubali  kushiriki  ligi  hiyo  lakini wachezaji hao wamebaini kuwa kulikuwa na njama iliyokuwa imeandaliwa na Viongozi wa MDFA na hawakutegemea kama timu hiyo ingeweza kufikia hapo ilipofika kwa kunyakua ubingwa wa Ligi ngazi ya Wilaya ya Misungwi kwa mwaka 2014.

Baada ya ushindi huo,Viongozi wa MDFA Wilaya ya Misungwi wanadaiwa kufanya mchakato wa  kubadilisha  ushindi wa Chitah FC kuwapa  ushindi huo kwa timu ya Halmashauli ya Wilaya ya Misungwi  Winners FC,ambayo  hata hivyo timu hiyo ilishika nafasi ya 4 kati ya timu 6 zilizoshiriki  ligi hiyo ikiwa na  point 7.
Huku Chitah FC wakimaliza ligi hiyo wakiwa  point 11.

Timu zilizoshiriki michuano hiyo ni  Chitah FC imefunga magoli 7 imefungwa magoli 2 Point 11 ,
Stand FC Misungwi imefunga magoli 7 kufungwa magoli 3 Point 8 ,
Brek FC ya Kijiji  cha Nguge imefunga magoli 7 imefungwa magoli 4 Pointi 7 ,
Misungwi Winners inayomilikiwa na Halmashauri ya  Wilaya ya Misungwi, imefunga magoli 11 imefungwa magoli 10 Point 7
Kwiki Sport Club ya Kijiji cha Wanzamiso imefunga magoli 4 imefungwa magoli 5 ina Point 7.
Vijana FC ya Kijiji cha Mapilinga imefunga magoli 3 imefungwa magoli 19 ina Point 0
Tanzania Daima ilipata nakala ya barua ya Chita FC ya tarehe 04 August 2014 kwenda Chama cha  Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza MZDFA iliyokuwa ikipinga ushiriki wa timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi katika ligi ya Mabingwa kwa kuwa haikuwa na sifa ya kushiriki ligi hiyo.

Wachezaji wa Chita FC wamekiomba Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza MZDFA kusaidia kusimamia haki na wahusika wachukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuwa vitendo hivyo vinazorotesha soka nchini.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment