Friday, August 8, 2014

Mwandishi anusurika kipigo cha OCD Geita.

<![endif]-->Mwandishi anusurika kipigo cha OCD Geita.
Na Antony Sollo Geita.

August 08.2014.

MWANDISHI wa habari wa gazeti la Tanzania Daima Wilayani Geita Valence Robart,amenusurika kupigo kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Wilaya ya Geita,OCD Busee Bwire,muda mfupi baada ya kufika kituoni hapo imefahamika.

Robart alifika kituoni hapo akifuatilia maendeleo ya kesi aliyoifungua kituoni hapo julai 23 mwaka huu baada ya kuibiwa pikipiki yake aina ya SUNLG yenye namba za usajili T305 BWV ambayo iliibiwa na watu wasiojulikana.

Tukio la kutishiwa kupigwa na OCD Bwire lilitokea Aug 5 mwaka huu majira ya saa nane na nusu mchana  muda mfupi baada ya Robert kuwasili kituoni hapo kwa lengo la kuonana na mpelelezi wa kesi yake GE/RB/4617/2014 ambayo ilifunguliwa kituoni hapo.

Mara baada ya kufika kituoni hapo Robert alianza kuzungumza na Mkuu wa Kituo cha Polisi Geita  Enock Rayi hapo mapokezi CRO, ghafla alitokea OCD Bwire ambaye kwa wakati huo alikuwa ofisini kwake.

“Unashida gani kituoni hapa?umefuata nini?”OCD Bwire aling’aka.

Robert alijibu kwa upole nilichofuata hapa ni huduma,yaani nimekuja kufuatilia maendeleo ya kesi yangu kufuatia kuibiwa kwa Pikipiki yangu.

Imedaiwa kuwa OCD Bwire alimtaka Mwandishi huyo kuondoka mara moja eneo la kituo hicho kabla ya kuagiza awekwe Mahabusu kitendo ambacho kilionyesha udhalilishaji kwa raia badala ya kutekeleza majukumu ya ulinzi wa raia kama lilivyo lengo na madhumuni ya kuanzishwa kwa Jeshi la Polisi .

“Ondoka hapa mara moja kabla sijakuweka sero,nitolee sura yako hapa mara moja’’alisikika OCD Bwire akimfokea Mwandishi huyo ambaye baada ya vitisho hivyo Robert aliondoka Kituoni hapo.

Tanzania Daima lilifuatilia sakata hilo na kubaini kuwa kuna msuguano mkali baina ya Mwandishi na OCD Bwire kwa kuwa mara kadhaa aliwahi kuripoti matukio mbalimbali yanayofanywa na Bwire. matukio ambayo yamepelekea kulidhalilisha jeshi hilo.

Imebainika kuwa matukio yaliyomuudhi Bwire ni kuripotiwa kwa tukio la kuangusha gari la Jeshi hilo alilokuwa akiliendesha yeye wakati likitokea katika kituo kidogo cha Polisi  nyarugusu likiwa na watuhumiwa ambao walitoroka baada ya ajali hiyo huku kazi hiyo akihodhi mamlaka ya uendeshawaji wa gari hilo.

Tukio lingine ni lile la kumshambulia Mkewe Taus Mashaka na kumuuma mdomo hali ambayo imepelekea mwanamke huyo ambaye pia ni askari Polisi kitengo cha Usalama Barabarani kutimkia nyumbani kwao singida.

Tanzania Daima lilipomtafuta OCD Bwire kuzungumzia madai ya kumtishia na kutaka kupiga Mwandishi Bwire alijibu kwa mkato “mimi sijui”  

Robert amemuomba Mkuu wa polisi nchini IGP Ernest Mangu kumwajibisha Askari huyo ambaye kwa siku za hivi karibuni amefanya kitendo kinachokinzana na masuala ya Haki za Binadamu ikiwemo ukatili wa Kijinsia kwa kumpiga mkewe huku akijua kuwa kufanya hivyo ni kosa na ni kimnyume na Maadili ya Jeshi hilo.

MWISHO.


0 comments:

Post a Comment