![](file:///D:\DOCUME~1\JOFLOC~1.LTD\LOCALS~1\Temp\msohtmlclip1\01\clip_image002.gif)
P. O. BOX 1288, MHUNZE-KISHAPU-SHINYANGA (TZ)
Mobile:+255
762 117 117 / +255 785 118 118
![](file:///D:\DOCUME~1\JOFLOC~1.LTD\LOCALS~1\Temp\msohtmlclip1\01\clip_image003.gif)
TAARIFA YA SNDF KUHUSU KAMPENI
YA ASASI ZA KIRAIA
KUSAMBAZA UELEWA WA RASIMU
YA PILI YA KATIBA YA JAMHURI
YA MUUNGANO WA
TANZANIA KANDA YA ZIWA- MKOANI SHINYANGA
2014.
Utangulizi
SNDF ni Shirika lisilo la Kiserikali lililosajiriwa
kwa mujibu wa sheria ya mashirika yasiyo ya kiserikali ya mwaka 2002 ambapo
shirika hili lilisajiliwa Sept 20 .2011.
Shirika hili linafanya kazi kwa kushirikiana na
Kituo cha sheria na haki za binadamu katika masuala yanayohusu utetezi wa haki
za binadamu.
Makao Makuu ya Shirika hili yapo Wilayani Kishapu
Mkoani Shinyanga
ASASI YA NSDF Inapenda
kutoa Taarifa juu ya
mpango wa AZAKI
kuandaa kampeni ya
kusambaza uelewa wa Rasimu ya
pili ya
Katiba ya Jamhuri
ya muungano wa Tanzania.
Mpango
huu ni mpango
ambao Umekuwa ni
Kipimo na Dira kubwa na
ni mtihani ulioweza
kuwapima Watanzania na kuelewa .
kama Iwapo walikuwa na
Uelewa kiasi gani
kuhusu katiba ya jamhuri
ya Muungano wa Tanzania
na uhusiano wa
zoezi la sasa kuhusu
Rasimu ya pili ya
Katiba ambapo zoezi hili Iimezua Zogo na
Mjadala Mkubwa Bungeni
Dodoma.
Awali
ya yote napenda
kuitambua kazi kubwa
iliyo fanywa kwa ushirikiano wa LHRC na Asasi 14 juu
ya kuandaa mpango
huu ambao ni mzuri ili
kuweza kupata Dira juu ya
uelewa wa rasimu ya Katiba kwa Watanzania
Kuhusu
historia kubwa katika
Nchi kwa kuwa zoezi
la kuandika katiba
ya Nchi Chini
ya Mamlaka yao ndiyo
linafanyika kwa mara ya
kwanza tangu Nchi
yetu ipate Uhuru
tarehe 9.Dec. 1961.
Lakini
pia napenda kutambua
kazi zilizofanyika awali
ikiwemo uteuzi wa Tume
ya mabadiliko ya
katiba. Tume ambayo iliteuliwa
na Mh. Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Jakaya
Mrisho Kikwete na
kumpa Uenyekiti wa Tume
hiyo Mh. Jaji
Mstaafu Joseph Sinda
Warioba.
Tume
hii Imefanya Kazi
yake kwa Weledi
mkubwa, imeweza kuisimamia
vyema sheria ya Mabadiliko ya
katiba Namba 83, ya
Mwaka 2011 na
kutimiza vizuri wajibu wake katika
kukusanya Maoni ya Wananchi,
kufanya utafiti, kuratibu na kuandaa
Rasimu ya kwanza na ya pili ya katiba.
Tumeshuhudia
jinsi tume ya Mh. Jaji, Joseph, Warioba ilivyofanya kazi, nzuri katika kutetea
Maoni na Mawazo yaliyotolewa
na Wananchi maoni ambayo ndiyo msingi
mkuu wa utungaji wa katiba ya kidemokrasia, inayoshirikisha
wananchi wote kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu.
Mchakato wa kuandika katiba mpya sio jambo dogo la
kubezwa, kuingiliwa na taasisi yoyote ile kwa lengo la kutetea maslahi binafsi
ya kundi hilo, bali ni ushirikishwaji wa wananchi na kuweka mbele matakwa yao
na kuyazingatia, jambo ambalo litawafanya waheshimu masharti yaliyomo katika
katiba hiyo.
Kwa dhati kabisa, nawapongeza Wabunge wa Bunge
Maalum la katiba ambao wako mjini, Dodoma wakiendelea na uchambuzi wa Rasimu ya
pili ya katiba ambapo na pia naomba watambue kuwa kuteuliwa kwao kuwakilisha
makundi mbalimbali kutaleta heshima tu iwapo wataweka mbele masilahi ya watanzania
badala ya kuweka mbele itikadi za vyama vyao, ubinafsi na watambue kwamba,mchakato wa
kukusanya Maoni ya Wananchi ,
kuhakiki kupitia Mabaraza
ya katiba ulifanyika
kwa uwazi na kwamba
Rasimu ya pili imebeba
utashi wa Wananchi, hivyo inahitajika,
hekima, busara zaidi
wakati wa mjadala na kupitisha
Rasimu ya pili ya
katiba.
Nchi
yetu imepitia hatua
mbalimbali tangu Uhuru na
baada ya Kuziunganisha
Nchi, Mbili yaani Tanganyika na Zanzibar, hivyo mapendekezo
yaliyomo kwenye rasimu
ya pili ya katiba yatakuwa
na uhalali na heshima kubwa
iwapo tu mawazo ya
Wananchi yatapewa nafasi
kuliko kuendekeza ushawishi
wa kiitikadi wa vyama vya
siasa na ubinafsi.
Baada
ya Bunge Maalum
la katiba kupitisha
rasimu hatua inayofuata
ni Wananchi Kuridhia Mapendekezo
yaliyotolewa na Bunge Maalum kwa
njia ya kupiga
kura.
Lakini pia kuna uhitaji
mkubwa wa kutoa
Elimu kwa Wananchi ili
waje kufanya kazi
hii kwa umakini mkubwa,huku
wakielewa vyema haki na wajibu wao katika ushiriki wao ili tuweze kupata katiba
nzuri itakayotuongoza kwa zaidi ya maika 50 ijayo.
MANUFAA YA KAMPENI YA KUSAMBAZA
UELEWA WA RASIMU YA PILI YA KATIBA 2014
Mpango wa LHRC na Asasi 14 uliozinduliwa kanda ya
magharibi tarehe 22 March 2014 huko Kigoma umeleta manufaa makubwa kwa Watanzania
kwani kabla ya kampeni na baada ya kampeni hii
viashiria vinaonyesha, jinsi mpango huu ulivyowavutia Watanzania na
kuwafanya wawe na hamu, ya kuelewa Rasimu ya pili ya katiba na mwendelezo wa hatua
ya mwisho ili kuona, iwapo Bunge litakuwa limetimiza matakwa yao kwa kuheshimu
mawazo na mapendekezo yao yaliyomo katika, Rasimu ya pili ya katiba.
PONGEZI:
Napenda kuwapongeza Viongozi wa Mkoa wa Shinyanga na
Wilaya zote kwa ushirikiano mkubwa toka kwao pamoja na watendaji wa Serikali, kwa
kusimamia na kuhakikisha kampeni hii
inawafikia Watanzania Mkoani Shinyanga bila vikwazo, huu ndiyo uzalendo
unaopaswa kuigwa katika maeneo mbalimbali nchi ili kutoa nafasi kwa Watanzania
kuweza kushiriki kikamilifu katika mchakato wa Utungaji wa Katiba Mpya jambo
ambalo ni la kihistoria katika nchi yetu.
Vilevile Pongezi hizi ziwaendee wanahabari wa
Vyombo mbalimbali nchini kwa mchango wao
mkubwa sana katika kuhabarisha na kuelimisha wananchi juu ya kampeni hii mkoani
Shinyanga na sehemu mbalimbali ,nina imani kuwa,zoezi hili likiendelea hivi
nchi nzima, uelewa wa Watanzania utaongezeka maradufu na zoezi la upigaji kura
kwa hatua ya mwisho baada ya kumalizika kwa mijadala ya Bunge maalumu kumaliza kazi yake wananchi
watapiga kura huku wakielewa ni nini wajibu wao katika hatua ya Mwisho.
Taarifa hii imeandaliwa na:
Antony Johnson Sollo,
Mkurugenzi wa,
Shinyanga NguvuKazi Development Foundation SNDF.
S.L.P 1288,
Kishapu,
Shinyanga.
Email sndfoundation@ymail.com
www.sndffoundation.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment