- Dereva adaiwa kugushi nyaraka na kuiba mafuta.
- Aandika vibali feki kwa magari manne lita 270.
Dereva mmoja wa Halmashauri ya Wilaya ya
Misungwi jina tunalo,anatuhumiwa
kutengeneza nyaraka kwa ajili ya kuchukua mafuta ya magari manne kwa lengo la
kuiibia Halmashauri.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa wizi huo ulifanyika kati ya tarehe 01/06/2014 na tarehe
5/06/2014 ambapo tarehe juni 01 haikuwa siku ya kazi na wala hakukuwa na
dharula yoyote iliyotokea kwa mujibu wa chanzo cha habari hii.
Imeelezwa kuwa Dereva wa Lori namba SM 3283
alitengeneza vibali feki vya mafuta ya magari manne kwa Invoice namba 000316 ya
juni 01 mwaka huu toka idara ya Afya akiomba kupatiwa mafuta aina ya Diesel
kiasi cha lita 60 kwa ajili ya kwenda kusambaza chanjo vijijini kwa kutumia
gari namba STJ 2505.
Kwa mujibu
wa mtoa taarifa imeelezwa kuwa Dereva huyo alikwenda kituo cha mafuta
cha Smat Usagara na kupewa mafuta hayo huku akiwa amegushi sahihi ya dereva
mwenzie J. malimi kwa mujibu wa nyaraka hiyo.
Siku ya tarehe 05 juni mwaka huu mtuhumiwa huyo
alitengeneza vibali vya magari matatu kwa kutumia invoice namba 001890 toka
idara hiyohiyo ya Afya akiomba mafuta aina ya diesel kiasi cha lita 210 kwa
kuyapangia kazi kama ifuatavyo, STJ 1189 lita 90 kwa ajili ya dharula ya
wagonjwa, gari ambalo liko kituo cha Afya Mbalika Wilayani Misungwi huku
akighushi sahihi ya dereva wa gari hilo Benjamini Bukindu.
Magari mengine ni SM 4774 lita 70 kwa ajili ya
shughuli za utawala,gari hili likielezwa kuwa dereva wake Makoye Mwilima alikuwa
mgonjwa kwa muda wa mwezi mzima na gari
lake lilikuwa limepaki.
Gari lingine ni STJ 4505 lita 50 kwa ajili ya
shughuli ya kusambaza chanjo vijijini gari ambalo haliko katika orodha ya
magari ya Halmashauri ya Wilaya hiyo.
Akiongea na Tanzania Daima kwa sharti la
kutoandikwa jina lake gazetini,dereva wa gari mojawapo linaloonekana
lilichukuliwa kibali cha kwenda kuchukua mafuta hayo amesema “nimesikitishwa sana na tukio hili kwakuwa
linajenga hisia mbaya kwa utumishi na ninaomba vyombo vya dola vichukue hatua
kwa mhusika kwa vile alikuwa na nia mbaya na sisi”.
Mwandishi wa Habari hizi alimtafuta Dereva huyo kutaka
kupata ufafanuzi wa tuhuma zilizotolewa dhidi yake kwa namba za simu ya mkononi namba 0759123924
ambapo alisema yuko Mkoani geita akiuguza mgonjwa na kusema kuwa “ndugu
mwandishi mimi niko Geita nauguza mgonjwa na gari langu liko kijijini linasomba
mchanga na mimi sipo Misungwi”
Mkurugenzi wa Wilaya ya Misungwi Nathan Mshana
amekiri kuwepo kwa tukio hilo na kusema kuwa baada ya kupata taarifa hizo
anazifanyia uchunguzi na mhusika akibainika na kosa hilo atachukuliwa hatua za
kisheria kwa kupelekwa kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichuke mkondo wake.
Mwisho
0 comments:
Post a Comment