Misungwi waomba Kuundwa kwa Wizara ya Wazee.
Na Antony Sollo
Mwanza.
June 18, 2014.
WAZEE
Wilayani Misungwi wameitaka Serikali kuunda Wizara ya Wazee nchini,ili kuweza
kusikiliza na kutekeleza sera ya huduma mbalimbali kwa wazee kama ilivyo katika
kundi la Vijana , kauli hiyo ilitolewa
na washiriki wa semina iliyokuwa imeandaliwa na Tume ya kurekebisha Sheria
iliyofanyika juni 17 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mkoani
Mwanza.
Ujio
wa Tume hiyo Jijini Mwanza ni kwa ajili ya kufanya utafiti na kukusanya maoni
juu ya mfumo bora wa sheria ya kusimamia huduma kwa wazee ambapo katika Mkoa wa
Mwanza. Wilaya zilizokuwa katika mpango huo ni Wilaya ya Misungwi na Nyamagana.
Tume
hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Aloyce Mujulizi,akifuatana na
wanasheria wa Tume hiyo Adamu Mambi,(Naibu Katibu),Bi Christina Binali
(Mwanasheria Mwandamizi wa Tume ) na Japhet Daud ambaye pia ni Mwanasheria wa Tume hiyo.
Akizungumza
na waandishi wa habari Wilayani Misungwi,Jaji Mujulizi alisema kuwa Tume hiyo
ilianzishwa chini ya kifungu cha 3 cha sheria ya kurekebisha sheria namba 11 ya mwaka 1980,ambpo sheria hii kwa
sasa ni sura ya 171 ya sheria za Tanzania toleo la mwaka 2002.
Jaji
Mujulizi alisema kuwa Tume hiyo ni Idara ya Serikali inayojitegemea chini ya
Wizara ya Katiba na sheria ambapo Tume hii ilianza kufanya kazi rasmi 21 Oktoba
1983 na kwamba tangu kuanzishwa kwake zaidi ya taarifa thelathini (30) zenye mapendekezo zimewasilishwa
Serikalini na tayari sheria mbalimbali zimefanyiwa marekebisho kutokana na
mapendekezo ya Tume hiyo.
Jaji
Mujulizi ameyataja majukumu ya tume hiyo kuwa ni kufanyia mapitio sheria zote
za Tanzania na kutoa mapendekezo ya marekebisho ,kwa kutathmini maeneo yote ya
sheria husika na kuyatolea mapendekezo kwa lengo la kuyaboresha,na baada ya
utafiti huo tume inapeleka ripoti kwa
Waziri wa sheria na Katiba kwa hatua zinazofuata.
Akiendelea
kutoa ufafanuzi kuhusu majukumu ya Tume hiyo,Jaji Mujulizi alisema
kuwa,mapendekezo ya Tume hiyo yamekuwa yakitiliwa maanani na serikali wakati wa
kutunga sheria na kanuni na kwamba serikali imekuwa ikitoa miongozo ya
kiutawala kutokana na mapendekezo ya Tume ili kuondoa kasoro zilizoainishwa na
wadau pamoja na Tume.
Katika
mada iliyotolewa juu ya utoaji huduma kwa wazee nchini Tanzania Elderly Social
Care in Tanzania,umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria ni miaka 60,lakini iko
wazi kwamba sio watu wote wenye umri huo na zaidi hawana nguvu za kufanya kazi
wakati huohuo baadhi ya watu wenye umri chini ya miaka 60 wanakuwa hawana uwezo
au nguvu za kufanya kazi.
Kwa
mujibu wa Mujulizi inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni 1.4 wana umri wa
miaka 60 na zaidi,na inakadiliwa kuwa ifikapo mwaka 2050 idadi itaongezeka na
kufikia watu milioni 8 kwa mujibu wa taarifa ya kabla ya sensa ya watu na makazi
ya mwaka 2002 na taarifa ya maendeleo Tanzania,mapitio ya MIPAA,katika kikao
kilichokaa Addis Ababa Ethiopia tarehe 19-21 Novemba 2007.
Jaji
Mujulizi alisema kuwa idadi kubwa ya wazee Tanzania wako kwenye matatizo
makubwa kwa sababu ya kutopata huduma na ulinzi mzuri Social and Security
Servises kwa kuwa wazee walioko kwenye mfumo rasmi ni wale walioko kwenye ajira
pekee,ambao hupata huduma katika mifuko ya jamii kama vile
NSSF,PPF,PSPF,NHIF,LAPF,GEPF ambapo mifuko hii hutunza akiba za wafanyakazi ( pensheni
) ambapo huwalipa baada ya kustaafu.
Kufuatana
na hali hiyo,Tume ya kurekebisha sheria nchini imeamua kufanya utafiti katika
eneo hili ili kubaini mapungufu yaliyopo kuhusiana na mfumo mzima wa utoaji
huduma kwa wazee Tanzania,kupitia mapungufu yake ili kufanyiwa maboresho na
katika hali hii Tume inakaribisha wadau mbalimbali kutoa maoni yao katika
kufanikisha zoezi hili alisema Jaji Mujulizi.
Wakichangia
mada hiyo,wazee hao walitoa mapendekezo mbalimbali ikiwemo kuwepo kwa dirisha
la huduma kwa wazee katika Halmashauri za Wilaya nchini ,kuundwa kwa taasisi
maalumu zinazotoa huduma kwa wazee, Benki,vyombo vya usafiri, nk ili
kuwaondolea usumbufu wazee nchini.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment