Wafugaji waichanganya Serkali.
Na Antony
Sollo.
CHAMA cha Wafugaji Nchini CCWT kimeichanganya Serikali baada ya
kuibuka kuwa makundi mawili yanayohasimiana na kusababisha mgororo mkubwa ndani
ya chama hicho.
Hayo yalibainishwa juzi na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dk Titus
Kamani wakati wa mkutano wake na waandishi wa Habari uliofanyika Ofisini kwake
mjini Dodoma.
Dk kamani aliiwaambia waandishi wa habari lengo la mkutano huo
lilikuwa ni kutolea ufafanuzi juu ya mambo mawili
,mgogoro kati ya wakulima na wafugaji uliotokea Mkoani Morogoro
pamoja na mgogoro unaofukuta ndani ya chama cha Wafugaji Nchini CCWT.
Akitoa ufafanuzi huo kwa waandishi wa Habari Dk Kamani alisema kuwa chama hiki kimesababisha
usumbufu mkubwa kwa wafugaji baada ya kuanzisha malumbano kati ya pande zote
mbili jambo linalowafanya wakose msimamo na imani na chama ambacho kilianzishwa
kwa lengo la kuwakomboa wafugaji hao.
Kuhusu kushamiri kwa matumizi ya risasi kwa makundi ya wakulima na
wafugaji wakati wa migogoro katika maeneo mbalimbali nchini Dk Kamani alisema
kuwa kumpiga mtu risasi ni kosa na huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine hivyo
alionya kuwa wote watakaobainika kufanya vitendo hivyo watachukuliwa hatua za
kisheria.
Waandishi wa Habari walipotaka kujua ni nini msimamo wa Dk Kamani
kuhusu mwaliko wa Jan 30 Dk Kamani
alisema kuwa hayuko tayari kuhudhuria Mkutano wowote wa chama hicho mpaka pale
watakapolipatia ufumbuzi suala hilo ili Kundi hilo liweze kupata uhalali wa
kutumia nembo na jina la Chama cha Wafugaji Taanzania CCWT.
Hata hivyo Mwenyekiti wa
chama cha Wafugaji Nchini CCWT taifa
Ally Lumiye alikiri kuwepo kwa makundi ndani ya chama hicho .
“ ni kweli kuna makundi ndani ya CCWT kuna kiongozi ambaye yuko katika kundi la
pili, huyu ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCWT George Kifuko ambaye alifukuzwa na
baadaye alifadhiliwa na wakala aliyepewa tenda na Wizara ya Mifugo kwa ajili ya
kusambaza madawa ya ruzuku,Gresso Bajuta ili kuchochea vurugu ndani ya Chama
cha Wafugaji ”.alisema Lumiye.
Akifafanua Lumiye alisema kuwa kabla ya kuibuka kwa mgogoro huo,Bajuta
alikuwa mjumbe wa bodi ya wadhamini wa chama cha Wafugaji na kubainisha kuwa
wakati chama kinamteua kuwa mjumbe wa bodi hiyo hawakujua kama Bajuta alikuwa
ndiye mmiliki wa Kampuni ya Bajuta International na ambayo ilipewa tenda na
Serikali kwa ajili ya kusambaza madawa ya ruzuku.
Imefahamika kuwa baada ya kufanya ziara nchi nzima, Mwenyekiti wa
CCWT Ally Lumiye alipata malalamiko toka kwa wafugaji kwamba hawapati madawa ya
ruzuku kabisa, baada ya ufuatiliaji ilibainika kuwa aliyekuwa amepewa tenda ya
kusambaza madawa hayo ni Bajuta International.
Kwa mujibu wa sheria ya
manunuzi PPRA hali hiyo ilipelekea ,mmiliki wa kampuni ya Bajuta International
Gresso Bajuta kukosa sifa ya kuwa mjumbe wa bodi ya wadhamini kutokana na
mgongano wa kimaslahi ya moja kwa moja.
Imeelezwa kuwa baada ya mtafaruku huo Gresso alianza kumfadhili aliyekuwa katibu Mkuu wa
CCW T George Kifuko kwa lengo la
kuchochea mgogoro na mgawanyiko ndani Chama hicho.
Kufuatia kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa CCWT Ally alisema kuwa Mkutano uliofanyika ukumbi wa
IRDP tarehe 24/25 mwaka huu ni halali na kwamba Mkutano huo ulitoa tamko la kuiomba serikali iingilie
kati mgogoro unaosababishwa na wakala anayelalamikiwa kutofikisha madawa ya
ruzuku kwa wafugaji.
Mkutano huo ulihudhuriwa na wanachama toka wilaya 17
zilizowakiliswa na wajumbe 4 pamoja na
wafugaji 120 kutoka nchi nzima walihudhuria huku Ally akizitaja Wilaya
zilizoshinikizwa kutoshiriki mkutano huo kuwa ni Bariadi,Meatu,Igunga na
Mkarama.
Tanzania Daima lilimtafuta Wakala wa Madawa ya ruzuku ambaye ndiye
mmiliki wa Kampuni ya Bajuta Inernational, Gresso Bajuta ili kutoa ufafanuzi
juu ya tuhuma za kuchochea mgawanyiko ndani ya CCWT ambapo alijibu kwa mkato kuwa yeye hana la
kuzungumza.
“Mimi sina la kuzungumza maana mimi si msemaji wa CCWT mimi ni
mjumbe wa bodi ya wadhamini wa muda,lakini pia mimi ni mfugaji tu hivyo kwa
haya unayoniuliza sina la kusema”.alisema Gresso.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment